Friday, May 27, 2016

Jose Mourinho atua rasmi Manchester United


 Manchester United leo imemtangaza Jose Mourinho kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo baada ya Mreno huyo kusaini mkataba wa miaka mitatu leo.

Jose Mourinho ametangazwa na klabu ya Man United  lakini atajiunga na kuanza kufanya kazi rasmi msimu wa mwaka 2016/2017 hii ina maana tutaanza kumuona Mourinho akiiongoza Man United  kama kocha mkuu wakati wa mechi za maandalizi ya mechi za msimu zitakazo fanyika nchini China.
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Jose Mourinho alifukuzwa kazi na Chelsea December 2015,  kocha huyo mwenye asili ya Ureno toka mwaka 2003 hadi sasa akiwa kama kocha amefanikiwa kushinda jumla ya Makombe 23 katika nchi 4 tofauti.

0 comments:

Post a Comment